Mkude aliumia dakika za mwisho za mchezo huo, na kusababisha kutolewa nje akiwa kwenye machela, ambapo baada ya kutoka pengo la nyota huyo lilionekana kutokana na safu hiyo kuanza kupwaya tofauti na awali.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mkude alisema, aligongana na mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngasa, mpaka kupata maumivu makali yaliyosababisha hasiweze kurudi tena dimbani.
Mkude alirejea hivi karibuni dimbani, baada ya kuwa majeruhi takribani wiki nne na kucheza katika mchezo huo ambao awali ulikuwa uchezwe Oktoba 12 na kusogezwa mbele.
CHANZO: TANZANIA DAIMA
0 comments:
Post a Comment