Muonekano wa uwanja wa Kaitaba unaotumiwa na Kagera Sugar katika michezo ya ligi kuu ya vodacom ukiwa katika uwekaji wa nyasi bandi |
Uwanja wa Kaitaba unatarajiwa kuwekwa nyasi bandi kama harakati hiyo inavyoendelea katika uwanja mwingine wa Nyamagana uliopo jijini Mwanza.
Kutokana na ukarabati huo michezo ya Kagera Sugar ambayo ilitakiwa kufanyika katika uwanja huo wa Kaitaba imehamishiwa katika uwanja wa CCM Kirumba uliopo Mwanza.
Kagera Sugar januari 17 wanataraji kuwakabili Mbeya City katika uwanja huo uliopo Mwanza kabla ya kuvaana na Azam FC januari 20 katika uwanja huo huo wa CCM Kirumba.
Picha na Faustine Ruta wa www.bukobasports.com
0 comments:
Post a Comment