VPL

KAGERA WAANZA KUCHINJA KAITABA, MBEYA CITY IKIUWA MWANZA

Wakatamiwa wa Kagera, Kagera sugar wameanza vyema kutmia nyasi mpya za bandia zilizopo katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera, baada ya kushindwa kuutumia uwanja huo, ambao ni nadra timu ngeni kuondoka na ushindi kwa misimu miwili iliyopita.

Kagera sugar hii leo wamefanikiwa kuwafunga Mwadui FC goli 1-0, goli lililofungwa na Ally Ramadhan na kuifanya Kagera kufikisha point 5 katika michezo 3 waliocheza.

Katika mchezo mwingine wa ligi kuu ya vodacom uliofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba umeshuhudia Mbeya city ikitoa kichapo cha goli 4-1 mbele ya wenyeji wao Mbao FC.

Katika mchezo huo Mbeya city waliandika goli la kwanza kupitia kwa Raphael Alfa katika dakika ya 21 kabla ya Mbao FC kusawazisha katika dakika ya 35 kupitia kwa Philipo Vicent.

Mbeya city walifunga magoli mengine matatu katika kipindi cha pili kupitia kwa Omary Ramadhan, Ramadhan Chombo na Raphael Alfa na kupelekea City kuibuka na ushindi wa goli 4-1.

Matokeo mengine, JKT Ruvu 0-0 AFRICAN LYON, MAJIMAJI 1-2 MTIBWA SUGAR

About dada

0 comments:

Powered by Blogger.