vilabu

GEOFREY MLAWA YUKO KATIKA HALI NZURI YA KUIKABILI PRISONS

Mkuu wa kitengo cha utabibu  kwenye kikosi cha City  Dr Joshua Kaseko amethibitisha kuwa mshambualiji nyota Geofrey Mlawa aliyetolewa nje baada ya kuumizwa na kipa John Kavishe wa JKT Ruvu kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulicheozwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya jana atakuwa sehemu ya kikosi kwenye  mchezo ujao dhidi ya Tanzania Prisons.

Akizungumza mapema leo Dr Kaseko amesema Mlawa hakuvujika mguu kama ambavyo taarifa zilizotolewa awali kupitia vyombo mablimbali vya habari isipokuwa mshambuliji huyo alipata mshituko mdogo kwenye kifundo cha mkuu wa kulia.

“Mlawa hakuvunjika mguu kama taarifa za mwanzo lizivyotolewa kilichotekea ni kwamba alipata mshituko kwenye kifundo cha mguu baada ya kipa wa JKT Ruvu kumkanyaga wakati akijiandaa kupiga mpira, kilichomsaidia  kutokuvunjika mguu ni kwa sababu alikuwa kwenye mwendo wa kasi, tumemfanyia matibabu ya haraka  na tayari yuko kwenye hali nzuri, imani yangu kuwa atakuwa sehemu ya kikosi kwenye mchezo wetu ujao dhidi ya Prison” alisema Dr Kaseko.

Geofrey Mlawa amejiunga na City msimu huu akitokea Kimondo Fc ya Mbozi  jijini Mbeya na tayari amekuwa mchezaji muhimu kwenye safu ya ushambuliaji.

CHANZO: mbeyacityfc.com

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.