ZGPL

Timu ya Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar  JKU imezidi kujiweka kileleni mwa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja baada ya jana kuwanyuka majeshi wa Kipanga bao 1-0 katika mchezo uliosukumwa ndani ya dimba la Amani hapa mjini Unguja.

Katika mchezo huo JKU hawakucheza vyema licha licha ya ushindi huo walioupata kwa penalt baada ya vuta nukuvute katika lango la Kipanga wakati JKU walipotaka kufunga bao, ndipo mwamuzi wa mtanange huo Issa Haji alipoamua ipigwe penalt.

Feisal Salum ndipo alipopiga penalt hiyo na mpira moja kwa moja kuingia wavuni katika dakika ya 79 ya mtanange huo.

JKU bado wanaendeleza ubabe wao wakiwa na alama 47, huku wanaowafukuzia ni timu ya KVZ ambayo wapo nafasi ya pili na alama 33, Kipanga wao wana alama 24 wakiwa nafasi ya nane 8.

Chanzo: salama sports media

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.