kitaa

TAARIFA KUU MBILI KUHUSU SIMBA NA MO ZILIZOIPOTIWA LEO MCHANA

Picha kutoka Boiplus blog ikionyesha baua kwenda kwa Mohammed Dewji kumuomba achangie  usajili

DEWJI AWASILISHA BARUA RASMI KUINUNUA SIMBA, AMUACHIA AVEVA OFISINI KWAKE

Blog ya salehjembe imeripoti kuwa:
Mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji amesema tayari ameandika barua kwa uongozi wa Simba kueleza kuhusiana na uamuzi wake wa kutaka kununua hisa za Simba kwa asilimia 51.

Mo amesema ameandika barua hiyo leo asubuhi baada ya kusikia baadhi ya viongozi wa Simba wakisema hakuwa amefanya hivyo.

"Kweli hatukuwa tumeandika barua kwa kuwa nilitaka mchakato uchukue hatua. Baada ya hapo lingefuata suala labarua, lakini kwa kuwa wanasema lazima barua, basi acha tufanye hivyo.

"Tayari barua imeandikwa na imepelekwa kwenye klabu, kukawa hakuna mtu na sasa imepelekwa ofisini kwa Aveva," alisema Mo.

"Nilichoeleza kwenye barua yangu ni kilekile kwamba ninatoa ofa ya Sh bilioni 20 ili kupata hisa asilimia 51. Niko tayari kushirikiana na uongozi wakati wa mchakati kama ambavyo nilieleza awali," alisema.
Picha ya baua aliyotumiwa MO kutakwa kukutana na kamati ya utendaji ya Simba SC (Picha kutoka kwa Boiplus Blog)

SIMBA YANUKIA MIKONONI MWA MO, ATAJA SABABU YA KUTOPELEKA OFA KWA MAANDISHI

Mtandao wa Shaffih Dauda umeripoti kuwa:
Ikiwa ni siku moja tu baada ya wanachama wa klabu ya Simba kuridhia mabadiliko ya klabu yao kutoka kwenye mfumo wa sasa wa uanachama hadi kuwa kampuni ambayo itaendeshwa kibiashara, bilionea Mohamed  Dewji leo amekutana na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba yuko tayari kuweka kitita cha bilioni 20 kwenye klabu hiyo ili amiliki 51% za hisa.

MO amewashukuru wanachama wa klabu ya Simba kwa kukubaliana kwa pamoja kuunga mkono mabadiliko ya kiuendeshaji kutoka mfumo wa uanachama kwenda mfumo wa kibiashara na kusema: “Ni lazima tuwafikirie wanachama kwasababu walitoa damu na jasho lao kwasababu timu yetu ya Simba kwahiyo ni lazima na wao wanufaike na huu mfumo mpya wa uendeshaji wa kibiashara.”

Afafanua hoja ya kutofikisha ofa kwa maandishi


“Viongozi wa Simba wanasema natangaza kwenye vyombo vya habari dhamira ya kuwekeza kwenye timu lakini sijawahi kuandika barua kwa uongozi kuhusu dhamira yangu ya uwekezaji kwenye klabu.”

“Nimeshakutana mara kadhaa na viongozi wa klabu hiyo, nimekutana na Rais wa Simba si chini ya mara tatu, wameshawahi kuja ofisini kwangu si chini ya mara tatu pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji na kujadiliana juu ya suala hili.”

“Sisi tulikuwa tunasubiri wanachama wa Simba waridhie mabadiliko ya mfumo, kwa kuwa wamesharidhia, leo asubuhi nimetuma barua kwa rais wa Simba kuwaambia niko tayari kuwekeza bilioni 20 kama watakubali kunipa 51% ya hisa na kufafanua namna ya pesa hizo zitakavyotumika ndani ya klabu.”

“Barua tayari ameshapata, sasa namuomba Evans Aveva tuweze kukaa pamoja na kamati ya utendaji na wataalam wangu kuona uwezekano wa kufanikisha hili jambo haraka iwezekanavyo.

Aahidi kupiga tafu usajili


“Simba ikiridhia kubadili mfumo mimi nitakuwa tayari kusaidia kwenye usajili, nini siyo mtu muongo ahadi yake ipo palepale nitachangia kwenye mfuko wao wa usajili lakini lazima wao viongozi waridhie. Kama wao wakinifuata na kuniambia tuko tayari, mimi niko trayari kuwapiga jeki.”

Nawashukuru sana wanachama wa Simba, nawaahidi nitawapigania mpaka na wao wapate hisa kwenye klabu na tutashirikiana bega kwa bega kuimarisha  Simba.

Tayari uongozi wa Simba umeshamuandikia MO barua ya kuhudhuria kikao pamoja na kamati ya utendaji siku ya Jumatatu August 15, 2016.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.