netball

SHYROSE AISAIDIA CHANETA

http://www.tanzaniasports.com/wp-content/uploads/2012/10/sh7-e1359928358549-722x400.jpg
MBUNGE wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji jana alifungua mashindano ya Netiboli Taifa na kuahidi kutoa zawadi kwa washindi watatu kwa kiasi cha Sh milioni 2.2 kwa ajili ya kuwahamasisha wachezaji kucheza kiushindani katika michuano hiyo.

Mashindano hayo yatakayomalizika rasmi Januari 13, mwaka huu yameshirikisha timu kutoka Dodoma, Tabora, Arusha, Ilala, Kinondoni, Temeke, Pwani na Mjini Magharibi huku nyingine zikishindwa kufika kutokana na sababu mbalimbali.
Akizungumza kwenye ufunguzi wa mashindano hayo, Bhanji alisema timu itakayofanya vizuri ya kwanza itaondoka na Sh milioni moja, ya pili Sh 700,000 na wa tatu Sh 500,000.

“Mikoa iliyofika imeonesha ari kubwa ya mchezo huu, mimi nawaahidi kuwa timu itakayofanya vizuri itapata zawadi,” alisema.

Alisema kuna haja kubwa kwa Kampuni na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuchukulia mchezo huo kama mpira wa miguu na kuungwa mkono.

Bhanji pia, aliahidi kushirikiana na Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) katika kushirikisha wadau wa michezo umuhimu wa mchezo huo kwa ajili ya kuwavutia kuupenda na kuusaidia.

Alisema ili mchezo huo uwe mzuri kuanzishwe programu maalumu za Shule za Msingi ambazo watoto watakuwa wakielimishwa umuhimu wa mchezo huo, na hatimaye wakue huku wakiwa wanaupenda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chaneta Anna Kibira alisema ukosefu wa fedha wanaokabiliwa nao na ushirikiano kutokana na vyama vya mikoani ndio ambao umesababisha ushiriki wa timu za mikoani kuwa chache.

CHANZO: HABARI LEO

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.