CECAFA

MICHUANO YAKIMATAIFA AMBAYO SIMBA ANGESHIRIKI YAHAIRISHWA


Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), limeahirisha michuano ya kuwania Kombe la nchi unakopita Mto Nile ‘Nile Basin Cup’.

Taarifa iliyotumwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicolas Musonye inasema kwamba wamepata taarifa za kuahirisha michuano hiyo kutoka kwa waratibu wakiwamo wenyeji Sudan.

Taarifa imesema wamekubaliana kuahirisha mpaka hapo watakapotangaza tena hivyo Simba iliyoteuliwa na TFF kushiriki michuano hiyo, imetaarifiwa kusubiri tarehe mpya ya mashindano.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.