netball

TIMU 6 ZAPANDA DARAJA

TIMU sita za netiboli zilizokuwa zinashiriki fainali za Ligi Daraja la Pili Taifa zilizomalizika jijini Tanga, zimepanda daraja, imeelezwa. Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta), Annie Kibira alisema timu hizo zitachukua nafasi ya timu sita zilizoshushwa daraja kutoka katika Ligi Daraja la Kwanza.

Kibira alizitaja timu zilizopanda daraja kuwa ni Magereza, Chuo cha Dar es Salaam, Sedico ya Mwanza, Halmashauri ya Jiji la Tanga, Lindi Queens ya Lindi, Kigoma Queens ya Kigoma na Korogwe Queens ya Tanga.

Wakati timu zilizoshuka daraja kwa sababu mbalimbali ikiwemo kushindwa kushiriki Ligi Daraja la Kwanza bila kutoa sababu ni Polisi Mbeya, mabingwa wa zamani Filbert Bayi, Magereza, Tumaini na Teachers Kinondoni.

Akizungumzia mashindano ya Ligi Daraja la Pili yaliyomalizika Tanga, Kibira alisema yalikuwa na msisimko wa aina yake ukiondoa kasoro ndogo ndogo za baadhi ya timu kuchelewa kufika kituoni.
Naye Mwenyekiti wa Filbert Bayi Foundation (FBF), Filbert Bayi alisema hivi karibuni kuwa kuivunja timu yao ya netiboli baada ya kubaini kuwa uongozi wa sasa wa Chaneta hauna nia ya kuuendeleza mchezo huo kimataifa baada ya kushindwa kushiriki mashindano yoyote ya kimataifa tangu uingie madarakani.

Alisema wao walianzisha timu hiyo kwa lengo la kuinua vipaji vya wachezaji kitaifa na kimataifa, lakini Chaneta imeshindwa kuipeleka timu katika mashindano yoyote ya kimataifa.

Chaneta imedai ukata umefanya ishindwe kuipeleka Taifa Queens katika mashindano ya mataifa Singapore, ya Afrika Malawi, mashindano ya vijana Botswana na ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia yaliyofanyika Gaborone hivi karibuni.


CHANZO: HABAR LEO

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.