mtazamo

MAMBO YALIYOJITOKEZA KATIKA USAJILI NDANI YA VILABU VITATU KATIKA NAMBA

Na Abdallah H.I Sulyaman (Msuni)


Usajili wa ligi kuu ya Tanzania bara inayodhaminiwa na vodacom, ulifungwa jana saa sita usiku huku kukishuhudia wachezaji mbalimbali wakiachwa na wengine wakitoka katika timu moja kwenda timu nyingine.

Sports In Bongo leo inakuletea matukio katika mfumo wa namba, yaliyojitokeza katika dirisha hili dogo la usajili.

0. IDADI YA MECHI ZA USHINDANI ZA DIARA

Kiungo raia wa Mali, Ismaili Diara aliyesajiliwa mwanzoni mwa msimu huu na mabingwa wa Tanzania bara baada ya kufanya majaribio na kufuzu, na katika dirisha hili ndogo jina lake limeondolewa katika usajili wa Azam FC bila ya kucheza mchezo hata mmoja wa mashindano.

Diara akiwa Azam Fcsamepata kucheza michezo ya kirafiki ya kujiandaa na msimuu huu wa ligi kuu ya Tanzania bara, na kushindwa kupenya kwenye kikosi cha azam FC mara baada ya ligi kuuanza na kukosa nafasi ya hata kukaa kwenye benchi la Azam FC katika michezo yote saba ya ligi kuu iliyochezwa mpaka sasa.

Nafasi ya Diara imechukuliwa na Muivory coast Pascal Wawa amabaye ni mlinzi wa kati.

1. EMERSON NA JAJA

Inakwenda kwa Wabrazili wa wili ambao wAmeondolewa katika kikosi cha yanga kwa sababu mbalimbali. Wabrazili hao ni Jaja na Emerson ambao wote walikuja nnchini kwa nyakati tofauti kuitumikia yanga sc.

Jaja alisajiliwa na yanga mwanzoni mwa msimu na kufanya vyema katika michezo ya kirafiki ambapo kila mchezo ambao yanga ilifunga goli lazima jina la Jaja liwemo, ila mambo yalikwenda vyongo katika ligi kuu, kwani ndanoi ya mechi 7 ameshinda goli 1 tu.

Jaja alisoma alama za nyakati na kuombwa mkataba wake usitishwe katika dirisha hili dogo na nafasi yake ikajazwa na kiungo toka Brazili Emerson ambaye nae ameshindwa ameshindwa kufikisha mwezi ndani ya yanga toka asaini mkataba wa mwaka mmoja.

Emerson amecheza mchezo mmoja tu wa kirafiki dhidi ya Simba SC kabla ya jana mkataba wake kusitishwa na kuchukuliwa mshambuliaji toka Burundi hamisi ambwe ndani ya anga.


2. WACHEZAJI WALIOSIMAMISHWA WAPELEKWA KWA MKOPO

Dirisha hili dogo limeshuhudia wachezaji wa wili waliokuwa wamesimamishwa na uongozi wa Simba SC Amiri Kiemba na aruna Chanongo wakitolewa kwa mkopo kwenda Azam FC na Stand united.

Amir Kiemba ameenda kwa mkopo Azam FC wakati Chanongo akitua Stand United kwa mkopo baada ya kutuumiwa kuhusika na matokeo mabovu ya Simba SC katika michezo minne ya awali ambayo Simba SC waliambulia sare.


3. VIPIMO VYA AFYA

Katika dirisha hili dogo la usajili tumeshuhudia kwa mara ya kwanza wachezaji wakifanyiwa vipimo vya afya kabla ya kusaini mkataba na klabu husika, ila si wachezaji wote waliosajiliwa ndio waliofanyiwa vipimo vya afya katika dirisha hili dogo la usajili bali ni wachezaji watatu tu ndio waliopitia katika vipimo vya afya nao ni Pascal Wawa aliyejiunga na Azam FC, Danny Ssenkuruma aliyejiunga na Simba SC na Kpah Sherman aliyejiunga na yanga.

4. INGIZO JIPYA LA WAGANDA

Dirisha hili dogo la usajili limeshuhudia ingizo la wachezaji 6 wakigeni kati yao nne ni raia wa Uganda, ambao wamejiunga na klabu ya Simba SC na Azam FC.

Wachezaji wengine ni kutoka Liberia ambaye ni Sherman aliyejiunga na anga na Muivory coast Wawa aliyejiunga na Azam FC.

Waganda hao wapya ni Saimon na Danny Sserkuma, Juuko Murshid waliojiunga na Simba SC na Brian Majegwa aliyejiunga na Azam FC.


5. IDADI YA WAGANDA

Baada ya Simba SC kuingiza wachezaji wa tatu toka Uganda na kupelekea kuwa na wachezaji watano wa toka Uganda katika kuhitimisha kwa ligi kuu ya msimu huu, kitendo ambacho kinaweza kikawa ni rekodi kwa klabu ya Simba SC kuwa na wachezaji wote wakigeni toka taifa moja.

Simba SC ina waganda Emanuel Okwi, Joseph Owino, Sserkuma wa wili na Murshid.


7. DANNY MRWANDA ABAKI BONGO

Mshambuliaji aliyejiunga na anga baada ya kucheza michezo saba na Polisi Morogoro Danny Mrwanda, alikuwa arejea nchini Vietnam lakini aliishia kutua yanga.

Danny Mrwanda baada ya kufanya vyema katika michezo hiyo 7 ya ligi kuu na kufanikiwa kufunga magoli 4, alivumishwa kujiunga na Simba SC mara baada ya kuwaaga mashabiki kwa ajili ya kwenda nchini Vietnam , lakini alirejea nchini na kujiunga na yanga sc.

Mrwanda alinukuliwa akisema kuwa alienda Vietnam kwa ajili ya majaribio kabla ya kupata majibu ya majaribio yake nchini Vietnam alipata ofa kutoka kwa yanga na kuamua kujiunga nayo.

Inadaiwa kuwa kabla ya kujiunga na polisi morogoro mwanzoni mwa msimu huu aliomba asajiliwe Simba SC lakini Simba ikamtolea nnje na kupelekea kujiunga na Polisi Moro.


8. MIKATABA YA WACHEZAJI YASITISHWA.

Imezoeleka dirisho dogo la usajili si wakati wa kusitisha mikataba lakini safari hii hali imekuwa tofauti baada ya mikataba 8 ya wachezaji kusitishwa, kata ya hiyo nane upo mmoja wa mchezaji wa ndani ambaye ni Uhuru Suleiman aliyekuwa naitumikia Simba SC.

Uhuru Suleiman aliomba mwenyewe mkataba wake usitishwe na viongozi wa Swimba kuridhia ombi lake na mkataba wake ukavunjwa bila ya malipo na kuenda kujiunga na Mwadui FC ya Shinyanga inayoshiriki ligi daraja la kwanza.

Mchezaji mwingine ambaye inasemekana aliomba mwenyewe mkataba wake uvunjwe na mshambuliaji wa yanga Jaja ambaye alii tumikia yanga kwa miezi minne tu na kuomba mkataba wake uvunjwe na uongozi kuridhia.

Mikataba mingine sita ni vilabu waliohusika katika uvunjaji wa mikataba ambapo azam FC ilisitisha mkataba wa Mhaiti Leonel na Mmali Diara, huku yanga waksitisha mkataba wa Emereson na amisi Kiiza na Simba SC waksitisha mkataba na Hamsi Tabwe aliyejiunga na yanga na Pierre Kwizera.

Huku kukiwa na taarifa ya Simba SC kumuondao bila ya kusitisha mkataba, kwenye usajili wao mshambuliaji aliyemajeruhi Patrick Kiongera ambaye anatarajiwi kurejea uwanjnani hivi karibuni.

About Unknown

0 comments:

Powered by Blogger.