mtazamo

AZAM MMENIANGUSHA

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na utamaduni ya kuuzwa tiketi zaidi ya uwezo wa uwanja katika michezo mbalimbali ya ligi kuu ya voadcom ambapo kumepatwa kushuhudia mashabiki wakishindwa kuingia uwanjani wakati bado wanatiketi zakuwa wezesha kuingia kushuhudia mchezo husika.

Hali hiyo ilitokea katika mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya vodacom msimu huu katika uwanja wa Jamhuri Morogoro kati ya yanga na Mtibwa sugar ambapo kunadaiwa kuna mashabiki walizuiwa kuingia baada ya uwanja kujaa wakati mashabiki walio nnje wakiwa na tiketi halali za mchezo huo.

Jana katika mchezo wa klabu bingwa Afrika kati ya Azam FC dhidi ya El-merekh uliochezwa katika uwanja wa Azam Complex kumeshuhdia tukio hilo likijirudia tena, la kushangaza zaidi siku nne kabla ya mchezo mtendaji mkuu wa Azam FC alikuwa akisikika akinadi kuwa tiketi zitakazo uzwa ni 7000 kulingana na uwezo wa uwanja wao.
Mashabiki walioshindwa kuingia uwanjani hapo jana
Kutokana na hali ilivyokuwa hapo jana kuna sitofahamu mbili zimejitokeza, ambazo ni nangoja majibu toka kwa uongzi wa Azam FC, mara baada ya kumalizi kujitathmini, katika uwandaaji wa mchezo huo wa jana. Sitofahamu hizo ni; Je uwanja wa Azam complex hauna uwezo wa kuchukua mashabiki 7000 ama tiketi ziliprintiwa zaidi ya 7000.

Kwa namna uongozi wa Azam FC unavyo jinadi kuwa na watu makini, kwa tukio la jana limepunguza asilimia za uaminifu toka kwa wadau wa mpira wa miguu nchini.

Ukiondoa uzembe huo uliojitokeza hapo jana, na kupelekea maelfu ya mashabiki waliokuwa nnje ya uwanja kukosa kushuhudia mchezo huo, hakukuwa na tatizo lolote lile kwa mchezo huo kuchezwa katika uwanja wa Azam complex.

Wachezaji wa Azam fc wanakuwa huru zaidi na kujihisi wako nyumbani pale wanapocheza michezo yao katika uwanja wa Azam complex kuliko wanapocheza taifa, na kwa anae juwa umuhimu wa mechi ya nyumbani kamwe. hawezi kuwalaumu Azam FC kuutumia uwanja wa Azam complex katika michezo mikubwa na muhimu kama huo wa jana.

Uongozi wa Azam FC wanatarajiwa kuwa makini wakati mwingine kwa kuhakikisha wanaprinti idadi sahihi ya tiketi kulingana na uwanja na kuondao mwanya wa udanganyifu unao weza kujitokeza na kupelekea hali kama hiyo kujitokeza.

Nawapongeza Azam FC na yanga sc kwa ushindi walio upata hapo jana na juzi katika michezo yao ya kimataifa.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.