maproo

TCHECHE KUREJEA UWANJNI BAADA YA SIKU 3

Taarifa zilizotoka kwenye benchi la kitabibu la Azam FC, zinasema kuwa Tchetche hajapata majeraha makubwa kama inavyodhaniwa katika mchezo uliopita dhidi ya Bidvest Wits.

Tchetche alipata majeraha ya enka dakika ya 88 mara baada ya kufunga bao la tatu akimalizia hat-trick yake Jumapili iliyopita dhidi ya Bidvest Wits, majeraha yaliyomfanya kushindwa kuendelea na mchezo huo na Azam FC kulazimika kucheza pungufu ya mchezaji mmoja hadi mpira huo unamalizika.

Akizungumza na mtandao wa rasmi wa klabu hii wa www.azamfc.co.tz Daktari wa Azam FC, Dr. Juma Mwimbe alisema kuwa Tchetche amepata majeraha madogo ambayo hayawezi kumfanya akose mechi zijazo za mabingwa hao wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la CECAFA Kagame).

“Anahitaji kupumzika kwa siku tatu tokea jana na baadaye ndio tutakiwa kumfanyia vipimo ili kuona kama atatakiwa kupumzika kwa muda gani au atatakiwa kuendelea na programu za mazoezi za kawaida, lakini majeraha aliyopata ni madogo hayawezi kumfanya akose mechi zijazo,” alisema.

About Unknown

0 comments:

Powered by Blogger.