Mchangani

LIGI DARAJA LA PILI YAENDELEA KARUME


Ligi Daraja la Pili (SDL) Tanzania Bara imeanza kuchezwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam kwa kuzikutanisha timu nne zinazowania kupanda kucheza Daraja la Kwanza (FDL), msimu wa 2016/17.

Timu hizo zilizoanza kuchuana Mei 11, zitacheza ligi hiyo hadi Mei 18, mwaka huu inazikutanisha Mvuvumwa ya Kigoma, Abajalo ya Dar es Salaam, Pamba ya Mwanza na The Mighty Elephant na mbili kati ya hizo zitakazofanya vema ndizo zitakazopanda daraja.

Taarifa ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), inasema michezo hiyo  zinazopigwa kuanzia saa 10.00 jioni, kiingilio chake kimepangwa kuwa Sh 1,000.

Ratiba ya ligi hiyo inaonesha;

Leo Mei 11, 2016 Abajalo v Mvuvumwa
         Mei 12, 2016 Pamba v The Mighty Elephant
         Mei 14, 2016 The Mighty Elephant v Mvuvumwa
         Mei 15, 2016 Abajalo v Pamba
         Mei 17, 2016 Mvuvumwa v Pamba
         Mei 18, 2016 The Mighty Elephant v Abajalo

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA), Nassibu Mabrouk ametowa wito kwa wakazi wa Mwanza kuichangia timu ya Pamba maarufu kama TP Lindanda iliyoko Dar es Salaam kwa sasa, ili iweze kufanya vema.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.