ZGPL

JKU WATOA SARE NA ZIMAMOTO, CHIPUKIZI IKITOA DOZI

Msimamo wa ligi kuu ya Zanzibar hatua ya nane bora baada ya michezo ya jana
JKU imebanwa mbavu na Zimamoto katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar hatua ya nane bora uliochezwa jana katika uwanja wa Amani kisiwani Unguja katika muendelezo wa hatua hiyo.

Katika mchezo huo Zimamoto walikuwa wa mwanzo kupata goli kupitia kwa Hakim Khamis katika dakika ya 17 kabla ya JKU kusawazisha katika dakika ya 44 kupitia kwa Emanuel Martin na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare ya goli 1-1.

Katika mchezo mwingine uliochezwa katika uwanja wa FFU Finya ulishuhduia Chipukizi wakiibuka na ushindi wa goli 4-1 mbele ya African Kivumbi.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.