vilabu

MAJIMAJI WA MWAGIWA NOTI NA SOKABET

Klabu ya Majimaji ya mkoani Ruvuma wamefanikiwa kupata udhamini toka katika kampuni inayojihusisha na mchezo wa kubashiri ya Sokabet  hii leo. Mkataba huo ukiwa ni wa mwaka mmoja.

Majimaji walinusurika kushuka daraja katika msimu uliopita, udhamini walioingia hii leo unathamani ya Tsh milioni 150 ambao utadumu kwa mda wa mwaka mmoja.

Katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Courtyard, Dar es Salaam, Mwakilishi wa kampuni hiyo nchini, Franco Ruhinda amesema kwamba Tanzania ni moja kati ya nchi inayopenda michezo hivyo wataipa kipaumbele michezo mbalimbali hapa nchini ikiwa wameanza na udhamini wa mwaka mmoja kwa Maji Maji.

About dada

0 comments:

Powered by Blogger.