TFF

TFF yakata matokeo ya Azam na Mtibwa


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema kuwa halitambui matokeo ya mchezo wa ligi kuu bara baina ya Azam Fc na Mtibwa Sugar uliochezwa jana katika Uwanja wa Azam ulopo Chamazi jijini Dar es Salaam.

Ofisa habari wa TFF, Boniface Wambura, ameiambia mamapipiro blog kwamba wamesikitishwa na hali iliyotokea, ambayo ilisababisha kutomalizika kwa mchezo huo uliokomea dakika ya 87, kwa matokeo ya sare ya bao 1-1.

Alisema, kanuni za mashindano hayo hazitambui matokeo ya mchezo unaovunjika, hivyo maamuzi rasmi kuhusiana na suala hilo, yatatolewa na Kamati ya Ligi, ambayo itakutana wakati wowote kuanzia sasa.


Source: Mamapipiro Blog

About kj

1 comments:

Kavishe said...

we need more update

Powered by Blogger.