Msimu huu wa ligi kuu ya Vodacom inayofikiwa tamati jioni hii, ambapo Simba SC imetwaa ubingwa, umeshuhudia mchezo mmoja kutoa mchezaji aliyefunga magoli matatu (Hart-trick) kabla ya michezo ya leo.
Hart-trick hiyo ilifungwa na JUMA SEMSUE anaevaa uzi namba 9 katika timu ya Polisi Dodoma iliyokwisha shuka daraja. Semsue alifunga magoli matatu katika mchezo baina ya Polisi Dodoma na Moro United.
Mchezo huo ulichezwa katika uwanja wa Azam uliopo Chamanzi jijini Dar es salaam, september 19 na Polisi Dodoma kutoka kifua mbele kwa goli 5-2.
Semsue msimu mzima amefunga magoli 6 kama Kipre Tchetche, Mrisho Ngassa wote wa Azam FC na Felixs Sunzu wa Simba SC, wakati John Raphael Bocco akiongoza list ya ufungaji kabla ya mchezo wa leo akiwa wamefunga magoli 17 ambayo ni ndoto kwa wachezaji walio chini yake kumfikia.
NO | JNO | GOAL SCORERS | GOALS TEAM | HTR | PNT | |
---|---|---|---|---|---|---|
1 | 19 | JOHN BOCCO | 17 | AZAM FC | 0 | 2 |
2 | 26 | KENNETH ASAMOAH | 10 | YANGA SC | 0 | 0 |
3 | 25 | EMMANUEL OKWI | 10 | SIMBA SC | 0 | 0 |
4 | 20 | HAMIS KIIZA | 10 | YANGA SC | 0 | 1 |
5 | 3 | NSA JOB | 10 | VILLA SQUAD | 0 | 2 |
6 | 30 | PATRICK MAFISANGO | 10 | SIMBA SC | 0 | 1 |
7 | 29 | SAID BAHANUZI | 7 | MTIBWA SUGAR | 0 | 0 |
8 | 27 | MOHAMED KIJUSO | 7 | VILLA SQUAD FC / RUVU SHOOTING | 0 | 2 |
9 | 11 | GAUDENCE MWAIKIMBA | 6 | MORO UNITED | 0 | 0 |
10 | 9 | JUMA SEMSUE | 6 | POLISI DODOMA FC | 1 | 0 |
11 | 16 | MRISHO NGASA | 6 | AZAM FC | 0 | 0 |
12 | 28 | DAVIES MWAPE | 6 | YANGA SC | 0 | 0 |
13 | 10 | KIPRE TCHETCHE | 6 | AZAM FC | 0 | 0 |
14 | 10 | FELIX SUNZU | 6 | SIMBA SC | 0 | 1 |
0 comments:
Post a Comment