TFF

TAIFA STARS WATOA SARE BOTSWANA

 
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imelazimisha sare ya kufungana mabao 3-3 na wenyeji Botswana mjini Gaborone katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa ulio kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
 
Katika mchezo huo, mabao ya Stars yalifungwa na Mwinyi Kazimoto, Erasto Nyoni ambaye baadaye alitolewa nje kwa kadi nyekundu na Mrisho Ngassa.
 
Stars inatarajiwa kurejea Dar es Salaam kesho baada ya mechi hiyo, na wachezaji wa timu hiyo kujiunga na klabu zao, kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

About kj

1 comments:

Anonymous said...

you hv a great sport website,but you always present insufficient details and information on topics you present!

Powered by Blogger.