Shirikisho la
Mpira wa Miguu na Vilabu vya Ligi Kuu wamo katika hali ngumu mno kifedha baada
ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kuzuia fedha za Shirikisho zilizoko kwenye akaunti
za TFF.
Jambo hili
limesababishwa na sakata la Kodi ya “PAYE” toka kwenye mishahara ya makocha wa
timu za Taifa wanaotoka nje ya nchi. Serikali iliyoko madarakani inayoongozwa na
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete
ilijitolea kulipia makocha wa kigeni, kuanzia kocha Maximo, Jan Poulsen na
wengineo.
Shirikisho la
Mpira wa Miguu wakiwa ndiyo wasimamizi wakuu wa mpira wa miguu hapa nchini,
ndiyo wanaongia mikataba na makocha hao, na malipo yanalipwa na serikali moja
kwa moja kwenye akaunti za makocha kupitia benki, hivyo nijukumu la serikali
kukata kodi ya “PAYE” kila inapopeleka mshahara.
Mamlaka ya Mapato
Tanzania wanalidai Shirikisho la Mpira wa miguu kiasi cha shilingi milioni
157,407,968.00 za Kitanzania, zikiwa ni kodi ya “PAYE” kuanzia kipindi cha kocha
Maximo na wengineo hadi sasa. Shirikisho la Mpira wa Miguu linapenda kueleza
kuwa uwezo wa kulipa deni hilo hatuna, vilevile makocha wa kigeni ni msaada
uliotolewa na serikali ya awamu ya nne katika kutimiza ilani yake ya uchaguzi.
Malipo kama tulivyoeleza yanalipwa moja kwa moja serikali kwenye akaunti za
makocha, hivyo suala hili linapaswa kamalizwa na pande pili za serikali kwa
maana Mamlaka ya Mapato na Wizara yetu husika.
Kitendo cha
Mamlaka ya Mapato Tanzania kuchukua fedha za Vilabu vya Ligi Kuu kutoka kwenye
akaunti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu, fedha ambazo zimetolewa na mdhamini wa
Ligi Kuu ya Vodacom kwa Vilabu vya Ligi Kuu, kitasababisha matatizo katika
uendeshaji wa Ligi. Jambo ambalo lingeweza kuepukika kwa pande zote kukaa chini
na kujadiliana kisha kufikia muafaka, kwani wanaoadhibiwa hapa ni vilabu.
Shirikisho kwa kushirikiana na Vilabu tupo kwenye mchakato wa kuunda kamati kwa
ajili ya kuonana na pande zote husika.
SUNDAY KAYUNI
KAIMU KATIBU MKUU
1 comments:
This is my first time pay a quick visit at here and i am truly happy to read all at alone
place.
Look at my webpage : Work from home jobs
Post a Comment