TFF

TFF LEO: VPL UKATA

Shirikisho la Mpira wa Miguu na Vilabu vya Ligi Kuu wamo katika hali ngumu mno kifedha baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kuzuia fedha za Shirikisho zilizoko kwenye akaunti za TFF.
 
Jambo hili limesababishwa na sakata la Kodi ya “PAYE” toka kwenye mishahara ya makocha wa timu za Taifa wanaotoka nje ya nchi. Serikali iliyoko madarakani inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ilijitolea kulipia makocha wa kigeni, kuanzia kocha Maximo, Jan Poulsen na wengineo.
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu wakiwa ndiyo wasimamizi wakuu wa mpira wa miguu hapa nchini, ndiyo wanaongia mikataba na makocha hao, na malipo yanalipwa na serikali moja kwa moja kwenye akaunti za makocha kupitia benki, hivyo nijukumu la serikali kukata kodi ya “PAYE” kila inapopeleka mshahara.

Mamlaka ya Mapato Tanzania wanalidai Shirikisho la Mpira wa miguu kiasi cha shilingi milioni 157,407,968.00 za Kitanzania, zikiwa ni kodi ya “PAYE” kuanzia kipindi cha kocha Maximo na wengineo hadi sasa. Shirikisho la Mpira wa Miguu linapenda kueleza kuwa uwezo wa kulipa deni hilo hatuna, vilevile makocha wa kigeni ni msaada uliotolewa na serikali ya awamu ya nne katika kutimiza ilani yake ya uchaguzi. 

Malipo kama tulivyoeleza yanalipwa moja kwa moja serikali kwenye akaunti za makocha, hivyo suala hili linapaswa kamalizwa na pande pili za serikali kwa maana Mamlaka ya Mapato na Wizara yetu husika.

Kitendo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania kuchukua fedha za Vilabu vya Ligi Kuu kutoka kwenye akaunti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu, fedha ambazo zimetolewa na mdhamini wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa Vilabu vya Ligi Kuu, kitasababisha matatizo katika uendeshaji wa Ligi. Jambo ambalo lingeweza kuepukika kwa pande zote kukaa chini na kujadiliana kisha kufikia muafaka, kwani wanaoadhibiwa hapa ni vilabu. Shirikisho kwa kushirikiana na Vilabu tupo kwenye mchakato wa kuunda kamati kwa ajili ya kuonana na pande zote husika.
 
 
SUNDAY KAYUNI
KAIMU KATIBU MKUU

About kj

1 comments:

Anonymous said...

This is my first time pay a quick visit at here and i am truly happy to read all at alone
place.
Look at my webpage : Work from home jobs

Powered by Blogger.