maproo

SAMATTA ATUPIA KATIKA USHINDI WA GOLI 4-0

Mshambuliaji wa kimataifa ya KRC Genk ya Ubelgiji raia wa Tanzania Mbwana Ally Samatta ameifungia timu yake goli la tatu katika ushindi wa goli 4-0 dhidi ya Oostende katika mchezo wa ligi kuu ya Ubelgiji.

Katika mchezo huo Samatta alianzia benchi ambapo aliingia katika dakika ya 75 kuchukuwa nafasi ya Kerelis na dakika moja baada ya kuingia mpira wake wa kwanza kugusa unaiandiki Genk goli la 3.

Katika mchezo huo Genk walikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2-0 ysliyofingwa na Alejandro Pozuelo katika dakika ya 12 na Thomad Buffel dakika ya 21.

Goli la 4 la KRC Genk  dhidi ya Oostend lilifungwa katika dakika ya 85 kupitia kwa Neeskens Kebano.

About dada

0 comments:

Powered by Blogger.