Mohamed Said Abdullah, Zanzibar
BAADHI ya mashabiki wa soka kisiwani Pemba wamekitaka Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), kuivua ubingwa timu ya Super Falcon baada ya kuitia kwenye makosa Kikwajuni kwa madai ya kuhusika na upangaji wa matokeo.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, mashabiki hao wamedai, adhabu dhidi ya Kikwajuni pekee bila Falcon, ni uonevu.
Kwa mujibu wa wadau hao, adhabu hiyo kwa Kikwajuni, mbinu ya viongozi kujisafisha kutokana na uendeshaji mbovu wa ligi ya msimu uliopita.
Wamedai kuwa madudu yaliyojitokeza ni baada ya ZFA-Pemba kushindwa kuwajibika kutokana na mizengwe iliyo kwenye chama hicho.
Khamis Mwinyi, alidai hata baadhi ya vifungu vilivyotumiwa na ZFA-Pemba kuiadhibu Kikwajuni, ni kutaka kujikosha kwa wadau dhidi ya utendaji wake.
Wameitaka ZFA kwenda mbali zaidi ya Kikwajuni kwa kuchukua hatua dhidi ya timu au watu walioshirikiana na Kikwajuni kupanga matokeo.
Meneja wa Jamhuri, Mohammed Abeid, aliishauri ZFA kuwa makini katika maamuzi yake, akiitaka kuzingatia sheria na kanuni.
ZFA Taifa Pemba iliishusha Kikwajuni madaraja mawili, kuifungia kucheza soka miaka miwili na kuitwanga faini kutokana na kukimbia mechi ya kumalizia msimu dhidi ya Jamhuri
BAADHI ya mashabiki wa soka kisiwani Pemba wamekitaka Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), kuivua ubingwa timu ya Super Falcon baada ya kuitia kwenye makosa Kikwajuni kwa madai ya kuhusika na upangaji wa matokeo.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, mashabiki hao wamedai, adhabu dhidi ya Kikwajuni pekee bila Falcon, ni uonevu.
Kwa mujibu wa wadau hao, adhabu hiyo kwa Kikwajuni, mbinu ya viongozi kujisafisha kutokana na uendeshaji mbovu wa ligi ya msimu uliopita.
Wamedai kuwa madudu yaliyojitokeza ni baada ya ZFA-Pemba kushindwa kuwajibika kutokana na mizengwe iliyo kwenye chama hicho.
Khamis Mwinyi, alidai hata baadhi ya vifungu vilivyotumiwa na ZFA-Pemba kuiadhibu Kikwajuni, ni kutaka kujikosha kwa wadau dhidi ya utendaji wake.
Wameitaka ZFA kwenda mbali zaidi ya Kikwajuni kwa kuchukua hatua dhidi ya timu au watu walioshirikiana na Kikwajuni kupanga matokeo.
Meneja wa Jamhuri, Mohammed Abeid, aliishauri ZFA kuwa makini katika maamuzi yake, akiitaka kuzingatia sheria na kanuni.
ZFA Taifa Pemba iliishusha Kikwajuni madaraja mawili, kuifungia kucheza soka miaka miwili na kuitwanga faini kutokana na kukimbia mechi ya kumalizia msimu dhidi ya Jamhuri
 

0 comments:
Post a Comment