OLJORO KUENDELEZA USHINDI MBELE YA SIMBA KESHO?

Baada ya kushindia katika michezo yake miwili ya awali iliyocheza katika uwanja wake wa nyumbani JKT Oljoro kesho watakuwa na kibarua cha kuendeleza wimbi hilo la ushindi pale watakapo wakaribisha mabingwa watetezi Simba sc katika uwanja wa Sh. Amri Abeid jikini Arusha.

Simba ambayo teyari wameshatua katika jiji la Arusha teyari kwa mchezy wa kesho watakosa huduma za mshambuliaji toka Zambia Felixs Muamba Sunzu watakuwa na kibarua cha kurejesha imani kwa mashabiki wake katika mchezo huo.

Mchezo wake wa mwisho wa ligi kuu ya vodacom simba walitoa sare ya kufungana goli moja kwa moja na JKT Ruvu katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Oljoro wamekuwa na matokeo mabaya wanapo kutana na simba katika michezo ya ligi kuu ya vodacom.


Wakati simba akiwa Arusha, Simba wa Afrika (African lyon) watakuwa Mbeya kusaka point 3 za kwanza chini ya kocha mpya Salum Bausi watakapo wakabili wanajera wa mjini hapo Prisons.

Mchezo huo kati ya Prisons na African lyon utachezwa katika uwanja wa sokoine mjini Mbeya.


MICHEZO MINGINE YA KESHO

KAGERA SUGAR Vs MGAMBO SHOOTING, Kaitaba

TOTO AFRICAN Vs COSTAL UNION, CCM Kirumba
--
MSUNI COMPUTER SOLUTION NDIO SULUHISHO LA COMPUTER YAKO
call us: +255-657-184-421
www.aboodmsuni21.blogspot.com

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.