POLISI MORO WAENDELEA KUJIKONGOJA WAPATA USHINDI WA PILI

Polisi morogoro ya Morogoro mjini wameendelea kujikongoja baada ya kufanikiwa kuwachapa goli 1-0 African lyon ya Mbagala jijini Dar es salaam na kufanikiwa kusogea kwa nafasi moja.

Polisi moro leo wamepata ushindi wake wa pili mfululizo katika michezo 15 ya ligi kuu ya vodacom na kufikisha point 10 ambazo zina mfanya atake mkiani (nafasi ya 14) ma sasa kushika nafasi ya 13 na kumuweka mkiani African lyon yenye point 9.

Lyon imeuwanza vibaya mzunguko wa pili kwa kukubali kufungwa michezo yote miwili ya duru la pili.

Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo uliwakutanisha Mgambo shooting na Ruvu shooting katika uwanja wa mkwakwani ambapo mchezo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana (0*0)

Ligi hiyo inataraji kuendelea kesho kwa michezo miwili kati ya SIMBA Vs JKT RUVU na COASTAL UNION Vs T.PRISONS
--
MSUNI COMPUTER SOLUTION NDIO SULUHISHO LA COMPUTER YAKO
call us: +255-657-184-421
www.aboodmsuni21.blogspot.com

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.