TFF

HABARI NJEMA KWA YANGA, MALINZI AFUTA MICHEZO YA KESHO

Raisi wa shirikisho la soka nchini Jamal Malinzi amefuta michezo yote ya ligi kuu ya Tanzania bara iliyokuwa ichezwe hapo kesho katika viwanja vya Taifa na Mkwakwani.

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kimataifa Yanga, kesho walikuwa na mchezo dhidi ya JKT Ruvu katika uwanja wa Taifa, wakati jumapili watakuwa na kibarua cha kuiwakilisha nchi katika kombe la shirikisho dhidi ya FC Platnum.

Mchezo mwingine wa kesho ulikuwa ni kati ya Azam fc na Mgambo shooting katika uwanja wa Mkwakwani.

Kuhairishwa kwa michezo hiyo kuna ipa muda zaidi wa yanga kujiandaa na mchezo wa kimataifa hapo jumapili, wakati azam fc wakielekeza maandalizi yao kwa mchezo dhidi ya Ndanda FC jumamosi.

About Unknown

0 comments:

Powered by Blogger.