MIEMBENI YAIONDOLEA AIBU ZFA, KUCHEZA NA TUSKER NUSU

Mabingwa wa zamani wa Zanzibar Miembeni fc jana iliondolea aibu waandaaji wa kombe la mapinduzu ZFA na kamati ya maandalizi ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya kufanikiwa kuwa timu pekee kutoka visiwani humu kutinga nusu fainali wakitoka suluhu na coastal union katika mchezo wa mwisho wa kundi B.

Hatua ya makundi ya kombe la mapinduzi ilihitimishwa jana kwa kushuhudia michezo yote miwhli ikimalizika kwa sare ya bila kufunganana.

Azam fc jana usiku walitoka sare ya bila kufungana na mtibwa sugar na kufanikiwa kuongoza kundi B ambapo ana kutana na mshindi wa pili wa kundi A ambaye ni simba sc

Miembeni wao jana jioni walitoka suluhu na coastal union ya Tanga na kufanikiwa kuwa wa pili katika kundi A ambapo watajabiliana na kinarara wa kundi B ambaye ni Tusker ya Kenya.

Micheyo ya nusu fainali itachezwa january 9 (TUSKER VS MIEMBENI) na january 10 (AZAM VS SIMBA).

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.