SIMBA WAPIGWA MATATU NA WANAJESHI

Mabingwa wa Tanzania bara Simba sc wamepokea kichapo cha goli 3-1 toka timu ya taifa ya jeshi la Oman linalo jiandaa kushiriki mashindano ya dunia yatakayo fanyika nchini Oman.

Katika mchezo wa jana uliochezwa katika nchi ya Omani ukiwa wa pili wa kirafiki kwa simba toka wawasili nchini humo, goli peke la simba sc lilifungwa na Haruna Moshi 'Boban'.

Huo ni mchezo wa pili kwa simba sc kupoteza baada ya kukubali kufungwa goli 1-0 na timu ya oliympiq ya Oman na kisha kupokea kichapo hicho cha goli 3-1.

Simba wako Oman kwa kambi maalum ya maandalizi ya ligi kuu ya vodacom na klabu bingwa Afrika.

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.