Timu ya taifa kwa soka la wanaume Taifa stars wamepoteza mchezo wao wa kirafiki jijini Addis Ababa, mbele ya wakilishi wa ukanda huu wa CECAFA katika michuano ya AFCON 2013 inayotarajiwa kuanza january 19 mchini Africa kusini, Ethiopia.

katika mchezo huo Ethiopia walikuwa wa mwanzo kupata goli katika dakika ya 15 kupitia kwa Fowad Ibrahim, goli lilidumu mpaka mapumziko.

Taifa stars walirejea kwa kasi katika kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha goli katika dakika ya 55 kupitia kwa Mbwana Samata na Waethiopia kuandika goli lao la ushindi kati dakika ya 83 kupitia kwa Shemele Nsekele kwa kichwa.

Hadi kipyenga cha mwisho kinapulizwa Ethiopia 2-1 Taifa stars

About kj

0 comments:

Powered by Blogger.